![]() |
Kikosi cha timu ya Azam fc wana lambalamba. |
Ushindi huo, sasa unakifanya kikosi cha Kocha
Stewart Hall kuhitaji japo sare ya aina yoyote ili kusonga mbele hatua
ya pili ya michuano hiyo.
Hata hivyo, pamoja na ushindi huo Azam inayocheza
kwa mara ya kwanza michuano ya kimataifa inayoandaliwa na Caf, wangeweza
kufunga mabao mengi zaidi hasa kipindi cha pili walichotawala mwanzo,
mwisho, huku kipa wa Nasri Peter Midia akiwa kikwazo kikubwa.
Katika mchezo huo, Abdi Kassim alifunga mara moja
kabla ya filimbi ya kutenganisha mchezo na Kipre Tchetche akaongeza
mawili kipindi cha pili.
Kipigo hicho hakikuonekana kumshtua kocha wa
Nasri, Ramzi Sebit kwani, mara baada ya mchezo alisema wanastahili
kupata ushindi mnono mechi ya
marudiano.
marudiano.
“Nimeona upungufu wa wachezaji wangu, nakwenda
kufanya marekebisho ili tushinde mechi ya marudiano,” aliwaambia
waandishi wa habari.
Abdi alibadilisha ubao wa matokeo na kusomeka 1-0,
baada mpira wake wa kichwa kulenga shabaha nyavu za Nasri kufuatia
krosi ya Kipre Tchetche dakika ya 14.Nasri, ambao nao wanacheza michuano
hiyo kwa mara ya kwanza baada ya Sudan Kusini kujitenga na Khartoum,
walisawazisha dakika ya 38 kupitia Fobian Elias kwa shuti.
Tchetche aliyekuwa mwiba ngome ya Wasudan hao,
aliwafurahisha mashabiki waliojitokeza uwanjani kushangilia kwa kufunga
bao la pili kwa kichwa dakika ya 80.
Kabla ya bao hilo, Tchetche alikaribia kufunga
kama siyo mpira aliopiga kukosa shabaha na kugonga ‘paa’ la goli la
Nasri dakika ya 54 kabla ya mabeki kuokoa.
Tchetche alikuwa hatari zaidi baada ya kuingia
John Bocco kuchukua nafasi ya Abdi, alikaribia kufunga dakika ya 60,
shukrani kwa kipa wa Nasri aliyefanya kazi nzuri. Bao la tatu la Azam
lilikuja dakika ya 90 kupitia tena kwa Tchetche aliyefunga kirahisi
akimalizia krosi ya Humphrey Mieno.
Kocha Hall, alisema amefurahishwa na matokeo hayo
na kwamba anajipanga kufanya marekebisho kwenye safu ya kiungo kwa ajili
ya mchezo wa marudiano.
Aidha, katika hatua nyingine suala la uzalendo
liliendelea kuwa ugonjwa nchini, kufuatia mashabiki wanaodhaniwa kuwa wa
Yanga kuishangilia Nasri iliyovaa jezi za njano.