Showing posts with label Teknolojia. Show all posts
Showing posts with label Teknolojia. Show all posts

Thursday, February 20

Unamjua Charles Robert Darwin?

Charles Robert Darwin (12 Februari 1809 - 19 Aprili 1882) alikuwa mwanasayansi Mwingereza katika karne ya 19.
Amekuwa mashuhuri kutokana na nadharia yake ya maendeleo ya uhai (mageuko ya spishi).
Nadharia hii yasema kuwa spishi zote za viumbehai vimetokana na spishi asilia zilizogeuka baada ya muda. Mageuko haya hufuata uteuzi asilia yaani viumbehai wanaolingana vizuri zaidi na mazingira wanaishi na kuzaa kushinda viumbehai wasiolingana nayo.
Kwa njia hiyo tabia za viumbehai wanaofaa vizuri zaidi zinazidi kuendelezwa kwa sababu watoto wao hurithi tabia hizi. Lakini tabia za viumbehai wasiofaa sana zinaweza kutoweka kwa sababu wanakufa mapema na hawana watoto wengi wanaoendeleza tabia zao.

Utoto na masomo


Alizaliwa mjini Shrewsbury (Uingereza) kama mtoto wa tano wa daktari Robert Darwin na Susannah Darwin (née Wedgwood).
Baada ya kumaliza shule alijiunga na chuo kikuu] cha Edinburgh (Uskoti) 1825 akajiandikisha katika idara ya tiba lakini hakupenda upasuaji. Alitumia muda mwngi kufuata kozi za biolojia, jiografia na jiolojia nje ya masomo ya tiba. Alifuatana mara nyingi na wataalamu walipofanya uchunguzi wa wanyama, mimea au mawe.
Baba baada ya kuona hafai kuwa daktari alimwandikisha katika masomo ya teolojia kwa shabaha ya kuwa mchungaji wa kanisa la Anglikanaaliyomaliza mwaka 1831.

Safari ya MS Beagle

Baada ya kumaliza masomo haya Darwin alipata nafasi ya kujiunga kama mshiriki na safari ya kisayansi ya jahazi MS Beagleiliyotakiwa kuzunguka dunia yote kwa kusudi la kuboresha ramani hasa za pwani la Amerika Kusini. Darwin alipewa nafasi ya mwanaviumbe bila malipo ya kuongozana na kushauriana na nahodha na kiongozi wa safari kuhusu wanyama na mimea visivyojulikana na vitakavyopatikana safarini.
Katika safari hii Darwin aliona Amerika Kusini na visiwa vya Pasifiki. Akaona mengi na kushika kumbukumbu yake akakusanya mimea na miili ya wanyama na kuibeba naye kwa ajili ya maonyesho katika jumba la makumbusha la historia ya viumbe.
Kwenye visiwa vya Galapagos aliona ya kwamba kila kisiwa kilikuwa na spishi za ndege pia kobe zilivyotofautiana kidogo kati ya kisiwa na kisiwa.

Mapinduzi ya kisayansi


aada ya kurudi Uingereza mwaka 1836 Darwin alianza kuchunguza sampuli zote alizokusanya. Alipata kazi kama katibu wa shirika la jiolojia.
Alipochungulia sampuli za Galapagos hasa alipata dhana ya kwamba spishi hizi zote za karibu zilitokana na aina moja tu iliyowahi kufika kwenye visiwa hivyo lakini baadaye zilianza kuwa tofauti katika kila kisiwa na kuwa spishi ya pekee. Kama hiyo ilikuwa kweli spishi hizi hazikuumbwa hivyo tangu mwanzo.
Darwin aliendelea na utafiti wa sampuli zake na kutoa masomo mbalimbali na kuyatafakari. 1859 alitoa kitabu kuhusu mageuko ya spishi kwa njia yauteuzi asilia (On the Origin of Species by Means of Natural Selection, or the Preservation of Favoured Races in the Struggle for Life) alimoeleza nadharia yake.
Kitabu kilikuwa kama bomu kati ya watu wa sayansi na wa dini.
Darwin alishambuliwa mara nyingi ya kuwa mafundisho yake yanapinga taarifa ya uumbaji katika Biblia. Lakini hiyo inategemea jinsi masimulizi yake yanavyosomwa: si lazima mwamini achukue kila kitu kama ilivyoandikwa, kwa sababu Biblia hailengi kutufundisha sayansi, bali njia ya wokovu.
Leo hii nadharia yake inakubaliwa na wanasayansi karibu wote hata kama bado kuna kiasi cha upingamizi dhidi yake kwa sababu za kisayansi na za kidini.

Wednesday, July 24

Mnajimu amegundua mwezi mpya unayozunguka Neptune

Inakadiriwa kuwa umbali wa kilomita 12 katika mduara, mwezi uko umbali wa kilomita 65,400 kutoka Neptune.
Mnajimu Mark SHOWALTER, na Taasisi Seti katika Mountain View, California, alikuwa akitafuta picha Hubble kwa mwezi ndani ya vipande kukata tamaa pete circling Neptune wakati yeye aliamua kukimbia uchambuzi wake juu ya sehemu ya mpango mpana wa angani.

"Sisi tulikuwa tunaendesha data hizi kwa muda mrefu kabisa na ilikuwa juu ya whim kwamba mimi nilisema, 'SAWA, hebu tuangalia nje zaidi," SHOWALTER aliiambia Reuters.

Nilibadili mpango wangu ili badala ya kuacha tu nje ya mfumo wa pete yake kusindika data njia yote nje, kutembea mbali na kompyuta yangu na kusubiri saa wakati ilivyokuwa usindikaji wote kwa ajili yangu. Wakati mimi nilipo rudi nyuma,  inaonekana katika picha na kulikuwa na dot ziada kwamba hakuwa walidhani kuwa huko, "SHOWALTER alisema.


Kufuatilia uchambuzi wa picha nyingine jalada Hubble ya Neptune kuthibitishwa kuwa kitu hicho kilikuwa ni mwezi.

SHOWALTER na wenzakewanatawa Kimataifa wa angani Muungano, ambayo ina kauli ya mwisho katika suala hilo.

"Sisi  kweli hatujafika mbali na kwamba Ninachoweza kusema ni kwamba jina litakuwa nje ya mythology Kirumi na Kiyunani.

wahusika ambao ni kuhusiana na Neptune, mungu wa bahari, "SHOWALTER alisema. Neptune mwezi kubwa, Triton, iligundulika mwaka 1846, siku chache tu baada ya sayari yenyewe kupatikana. Nereid, Neptune mwezi wa tatu kwa ukubwa ulipatikana mwaka 1949.


Picha zilizochukuliwa na spacecraft NASA Voyager 2 zilizindua dira ya pili kwa ukubwa mwezi, Proteusna watano mwezi ndogo, Naiad, Thalassa, Despina, Galatea na Larissa.

Ardhi makao darubini kupatikana Halimede, Laomedeia, Sao na Nestor mwaka 2002. Dada mwezi Psamathe akageuka hadi mwaka mmoja baadaye.


Paleontologists wamegundua mabaki ya mkia wa dinosaur kaskazini mwa Mexico

MEXICO CITY - Timu ya paleontologists wamegundua mabaki ya mkia wa dinosaur yenye umri wa mika milioni 72 katika jangwa  askazini mwa Mexico, Taasisi ya Taifa ya Anthropology na Historia (INAH) ilisema Jumatatu.
Mbali ya kutohifadhiwa  vizuri, mkia huo una mita 5 (16 mguu) mkia huo ni mara ya kwanza kuwahi kupatikana katika Mexico, alisema Francisco Aguilar, mkurugenzi wa INAH katika mpaka wa Coahuila.

Timu, inaloundwa na wanafunzi kutoka paleontologists INAH na ya Taifa ya Chuo Kikuu cha Autonomous Mexico (UNAM) kutambuliwa mafuta kama hadrosaur, au bata-billed dinosaur.



Mkia, ulipatikana karibu na mji mdogo wa eneo la Cepeda, mkia huo unaundwa nusu ya urefu wa dinosaur  Aguilar alisema.

Paleontologists iligundua vertebrae 50 ya mkia  baada ya kukaa siku 20 katika jangwa polepole huku wakiondoa mwamba wa sedimentary uliofunika mifupa ya kiumbe hicho.
Strewn wakauzunguka mkia wengine  fossilized mifupa, ikiwa ni pamoja na moja ya makalio dinosaur wa, INAH alisema.

Mkia wa Dinosaur huupata nimara chache sana, kulingana na INAH. Ugunduzi mpya unaweza zaidi ufahamu wa familia hadrosaur na utafiti juu ya misaada ya magonjwa ya kwamba taabu dinosaur mifupa, ambayo inafanana ile ya binadamu, Aguilar alisema.

 Wanasayansi tayari wamesema kwamba dinosaurs alikuwa nanaumwa na uvimbe na arthritis.

Mabaki ya dinosaur yamepatikana katika maeneo mengi ya hali ya Coahuila, pamoja na mataifa mengine ya Mexico kaskazini mwa jangwa.
"Tuna historia tajiri sana ya paleontolojia," Aguilar alisema.

Alibainisha kwamba wakati wa kipindi Cretaceous, iliyomalizika kuhusu miaka milioni 65 iliyopita, sehemu kubwa ambayo sasa ni kati ya kaskazini mwa Mexico ilikuwa pwani. Hii imewezesha watafiti kufukua vyote, dinosaurs wa baharini na nchi kavu-msingi.

Tuesday, July 23

Teknolojia ya habari na mawasiliano.

Teknolojia ya habari (information technology, IT), kama ilivyoainiwa na Shirikisho la Teknolojia ya habari ya Marekani (ITAA), ni "utafiti, urasimu, uendeleshaji, utekelezaji, usaidizi au usimamizi wa mifumo ya habari hasa ala za programu na vifaa vya kompyuta."  IT inahusika na matumizi ya kompyuta zitumiazo umeme na programu za kompyuta kubadili, kuhifadhi, kulinda, kuchecheta, kueneza, na usalama katika kupokea habari.
Leo, neno habari limezunguka nyanja nyingi za kompyuta na teknolojia, na neno hili limekuwa maarufu sana. Wataalamu wa IT hutekeleza jukumu mbalimbali kutoka kuweka ala hadi kubuni mitandao tata ya kompyuta na hifadhidata. Machache kati ya wajibu ya wataalamu wa IT ni kufanya usimamizi wa data, kujumuisha kompyuta ili kutengeneza mtandao, uhandisi wa hifadhidata na programu na vilevile usimamizi na utawala wa mfumo mzima.
Wakati kompyuta na teknolojia za mawasiliano zinapounganishwa, matokeo ni teknolojia ya habari, au "infotech". Teknolojia ya habari ni neno la jumla linaloelezea teknolojia yoyote ambayo husaidia katika kuzalisha, kuendesha, kuhifadhi, kuwasilisha, na / au kusambaza habari. Kwa makadirio, wakati tunapozungumza kuhusu teknolojia ya habari (IT) kama ujumla, ni bainisho kuwa matumizi ya kompyuta na habari yanashirikiana.
Katika siku za majuzi ABET na ACM wameshirikiana kuunda kanuni za akredishon na mitaala ya shahada katika teknolojia ya habari kama uwanja wa masomo uliotofautiana na Sayansi ya kompyuta na pia mifumo ya habari. SIGITE ni kikundi cha kazi cha ACM kilichopewa jukumu la kuweka kanuni hizi.

Monday, July 22

Sayari.

Sayari za jua letu.

Jua letu lina sayari nane ambazo ni Utaridi (Mercurius), Zuhura (pia: Ng'andu; Venus), Dunia yetu (Earth), Mirihi (Mars), Mshtarii (Jupiter), Zohali (Saturnus), Uranus na Neptun. Toka mwaka 1930 hadi Agosti 2006 Pluto ilikuwa ikitambulika kama sayari hivyo kufanya idadi ya sayari zinazojulikana kuwa tisa. Hata hivyo chama chenye mamlaka ya masuala ya sayari na nyota, International Astronomical Union kimetangaza rasmi kuwa Pluto sio sayari na kuiita sayari kibeti.
Sayari tano za Utaridi, Zuhura, Meriki, Mshtarii na Zohari  huonekana kwa macho kama nyota angani. Lakini tangu zamani zilitambuliwa kuwa tofauti kwa sababu hazikai mahali palepale kama nyota ya kawaida bali huhamahama angani. Kutokana na tabia hii zimetazamiwa mara nyingi kuwa na nguvu za pekee au hata kuwa miungu. Unajimu imetumia mwendo wa sayari zinazoonekana kwa macho kama msingi muhimu wa makadirio yao.
Sayari nyingine katika mfumo wa jua zimetambuliwa tangu kutokea kwa astronomia ya kisayansi kwa darubini. Hizi ni Uranus na Neptun. Katika lugha ya Kiswahili sayari zinazoonekana kwa macho huwa na majina ya asili ya Kiarabu isipokuwa Zuhura ina jina la Kibantu la Ng'andu pamoja na jina la asili ya Kiarabu. Majina mengine ni ya asili ya Kilatini.
Jumla ya jua, sayari zote 8 pamoja na miezi yao, sayari kibete, vimondo, nyotamkia na asteroidi inaitwa mfumo wa jua.

  • Aina za sayari.

Sayari za jua letu hutofautiana kati yao katika ukubwa na pia muundo. Mshtarii ni sayari kuwba na masi yake ni mara 318 masi ya dunia yetu. Sayari ndogo ni Utaridi na masi yake ni takriban nusu ya dunia.
Kutokana na umbali tunatofautiana "Sayari za ndani" kuanzia Utaridi (Mercurius) hadi ukanda wa asteroidi , halafu sayari za nje kuanzia Mshtarii (Jupiter) hadi Uranus.
Muundo ya sayari ni tofauti kuna vikundi kulingana na mata inayojenga sayari:
  • Sayari za mwamba: sayari hizi zina muundo unaofanana na dunia yetu; asilimia kubwa ya masi ni mwamba. Hizi ni sayari za ndani za mfumo wa jua letu. Zote ni ndogo kuliko sayari za nje.
  • Sayari jitu za gesi: Sayari hizi kama Mshtarii (Jupiter) na Zohali (Saturnus) ziko kubwa na zimefanywa na hidrojeni na heli. Masi ya Mshtarii ni mara 318 ile ya dunia, Zohali mara 95. Ilhali sayari hizi ni baridi kutokana na umbali mkubwa na jua hidrojeni inatokea kwa kiasi kikubwa katika hali mango na kwenye sehemu za ndani hidrojeni ina tabia kama metali kutokana na shindikizo kubwa.
  • Sayari jitu za barafu- hizi ni Uranus na Neptun. Ziko kubwa kuliko dunia lakini si kama sayari jitu za gesi; Uranus huwa na masi 14 za dunia, Neptun na masi 17 za dunia. Ganda la nje ni mchanganyiko wa hidrojeni na methani, na sehemu za ndani ni barafu ya maji na methani.
  • Sayari nje ya mfumo wa jua letu.

    Wataalamu wa astronomia wamegundua sayari hata nje ya mfumo wa jua letu zinazozunguka nyota mbalimbali. Kutokana na umbali mkubwa na matatizo ya utazamaji hakuna uhakika hadi sasa kama nyota kuwa na sayari ni jambo la kawaida angani au kama sayari ni chache tu. Lakini uwezekano ni kubwa ya kwamba sayari ziko nyingi sana.
    Hadi desemba 2012 jumla ya sayari 854 nje ya mfumo wa jua letu zimetambuliwa. Nyingi kati ya hao zilikuwa na ukubwa kufanana na Mshtarii au kubwa zaidi. Lakini sayari ndogo zaidi zimetambuliwa pia.

Ijue Computer ( Tarakilishi ). Sehemu ya III

Kompyuta imegawanyika katika sehemu kuu mbili:

I. Sehemu zinazoshikika (Hardware)
  Sehemu zinazoshikika (Hardware), ni aina zote za vifaa vya kompyuta, navyo vimegawanyika katika sehemu kuu tatu.

Vifaa vya kuingizia vitu (Input devices):
  1. kibodi (keyboard)
  2. Mausi (Mouse)
  3. Skana (Scanner)
  4. Makrofoni (Microphone)
  5. Kamera (Camera)
1. KIBODI (KEYBOARD):
Kibodi inatumika kwa ajili ya kuingizia herufi, namba, alama na michoro, nayo imegawanyika katika sehemu kuu nne, nazo ni kama ifuatavyo: Funguo za kuandikia (Typewriter keys), funguo za kuhama (Movement keys), funguo za namba pamoja na michoro mingine (Numeric keys) na funguo za kazi Function keys).

JEDWALI LINALOONYESHA FUNGUO NA KAZI ZAKE:
Jina la funguo Kazi yake Home Inatumika kwa ajili ya kuhamia mwanzo wa mstari End Inatumika kwa ajili ya kuhamia mwisho wa mstari.
Inatumika kwa ajili ya kuhamia juu ya mstari.
Inatumika kwa ajili ya kuhamia upande wa kushoto mwa mstari.
Inatumika kwa ajili ya kuhamia upande wa kulia mwa mstari.
Inatumika kwa ajili ya kuhamia chini ya mstari. Pg Up Inatumika kwa ajili ya kuhamia juu ya mstari. Pg Dn Inatumika kwa ajili ya kuhamia chini ya mstari. Num lock Inatumika kwa ajili ya kufunga na kufungulia namba na michoro. Caps lock Inatumika kwa ajili ya kufunga na kufungulia. Enter Inatumika kwa ajili ya kutekeleza amri, au kuanzisha fungu la maneno kwenye ukurasa.. Del “Delete” Inatumika kwa ajili ya kufuta herufi ya mbele yake.
“Back space" Inatumika kwa ajili ya kufuta herufi ya nyuma yake. Space “Space bar” Inatumika kwa ajili ya kuweka masafa kati ya maneno. Esc “Escape” Inatumika kwa ajili ya kuacha kutekeleza amri. Tab Inatumika kwa ajili ya kuwacha masafa maalumu tofauti na ya kawaida (Normal).
Ctrl “Control” inatumika daima pamoja na ufunguo mwengine kwa ajili ya kutekeleza amri maalumu. Alt inatumika daima pamoja na ufunguo mwengine kwa ajili ya kutekeleza amri maalumu. Shift inatumika daima pamoja na ufunguo mwengine kwa ajili ya kutekeleza amri maalumu. Alt-Shift Inatumika kwa ajili ya kubadilishia lugha. Ctrl-Shift Inatumika kwa ajili ya kubadilishia mwelekeo ndani ya ukurasa (kulia au kushoto) Print screen Inatumika kwa ajili ya kupiga picha kitu chochote kwenye kompyuta.
Ctrl-Alt-Del Inatumika kwa ajili ya kuwasha upya kompyuta.

3. MAUSI (MOUSE):
Kuna vitufe viwili kwenye kila mausi, kitufe cha upande wa kushoto (Left click) kinatumika kufungulia windozi, programu na kuchagulia maandishi, maneno na picha, na kitufe cha upande wa kulia (Right click) kinatumika kufungulia orodha ya mapendekezo ya kazi.

4. SKANA (SCANNER)
Skana inatumika kwa ajili ya kuingizia picha ndani ya kompyuta. Na kitu chochote kile kinachoingia ndani ya kompyuta kwa njia ya skana kinapewa sifa ya picha.

5. MAKROFONI (MICROPHONE):
Makrofoni inatumika kwa ajili ya kuingizia sauti ndani ya kompyuta.

6. KAMERA (CAMERA):
Kamera inatumika kwa ajili ya kupigia picha na kuingiza ndani ya kompyuta.

Viafaa vya kutolea vitu (Output devices):

1. SKRINI (SCREEN):
Skrini inatumika kwa ajili ya kuonyeshea matokeo ya vitu vilivyofanyika ndani ya kompyuta.

2. KIPAZA SAUTI (SPEAKER):
Kipaza sauti kinatumika kwa ajili ya kutolea sauti kutoka ndani ya kompyuta.

3. PRINTA (PRNTER):
Printa inatumika kwa ajili ya kutolea vitu vya maandishi au picha kwenye kompyuta kwa njia ya karatasi (kuchapisha).

4. PLOTA (PLOTER):
Plota ni ni chombo kinachotumika kwa ajili ya kutolea vitu, ambacho kinafanana na printa katika ufanisi wake wa kazi, lakini umbile lake ni kubwa kuliko printa, na kinatumika kwa ajili ya kuchapishia picha na michoro ya kiufundi, pia kinaweza kutumika kwa ajili ya kuchapisha maandishi kama herufi namba na alama.

II. Sehemu zisizoshikika (Software):

Kompyuta haiwezi kufanya kazi mpaka kipatikane kitu kinachoitwa software, ambocho kinawakilisha programu zinazoendesha kompyuta. Na programu hizo zimegawanyika katika sehemu kuu mbili:-
1. Programu za kuendeshea kompyuta (operating systems), programu hizo zinaitwa windows, na kuna aina nyingi za windows kulingana na toleo lake na ubora wake, kwani kila siku zinavyozidi kwenda mbele ndipo tunapozidi kupokea programu nyingine za windows na zenye ubora zaidi kuliko zile zamani.
2. Programu za kufanyia kazi (application systems), nazo ni Microsoft Office na Graphics design, programu hizo daima zinafanya kazi ndani ya windows, ambazo zinatumika kwa ajili ya kazi mbali mbali za uandishi na hesabu, na kazi nyenginezo za kuunda na kutengeneza picha n.k.

vifaa vya kuendeshea vifaa vya kuingizia na kutolea vitu:

Vifaa hivi vipo ndani ya chombo kiitwacho (C.P.U) kifupi cha Central Processing Unit, ambacho ni kiini cha kompyuta na ndicho kinachofanya kazi ya kuviendesha vifaa vyote vya kompyuta na kutoa maelekezo yote. Na C.P.U. ni sehemu kuu ya nguvu ya kompyuta, au kitovu cha kompyuta.
Kazi za C.P.U:

1. Kutawala (Control): Ndani ya madhabodi (Motherboard) kinapatikana kifaa kinachoitwa (Bios) kifupi cha Basic Input Output System, ambacho ndicho kinachofanya kazi ya kuviendesha vifaa vya kuingizia na kutolea vitu. Na ni vigumu kufuta au kurekebisha vitu vilivyomo ndani ya kifaa hicho kwani vinazingatiwa ni vitu vya kusomea tu na si kwa kazi nyingine.

2. akili na mahesabu (arithmetic logical):
Kazi za mahesabu ni kazi zote zinazofanyika na hesabu, kama vile kutoa, Kujumlisha, kuzidisha na kugawanya. Na za akili

WINDOWS XP:

Windows Xp inazingatiwa kuwa ni miongoni mwa Windows za kisasa zenye kufanya kazi kwa ufanisi zaidi kuliko zile za zamani, kama Windows 95, Windows 98 na Windows Millenium.

SIFA ZA WINDOWS XP:
  1. Uwepesi wa kuanza na kumaliza kutumia.
  2. Uwezo wa kutumia lugha mbili mfano kingereza na kiarabu, pia uwezo wa kubadilisha lugha hizo na kuweka nyengine.
  3. Kufungua kurasa kwa haraka.
  4. Uwezo wa kuendesha programu zaidi ya moja katika wakati mmoja.(Multitasking)
  5. Uwezo wa kuhifadhi vitufe (files) vilivyofutwa katika recycle bin.
  6. Uwezo wa kufanya kazi katika mdahalishi (Network) kwa haraka.
  7. Uwezo wa kubadilishana vitu (Data) kati ya programu tofauti.
  8. Kutumia majina marefu zaidi ya herufi 255 katika jina la faili moja.
  9. Haraka na uwepesi katika utekelezaji.
  10. Vifaa vya kisasa vinavyowezesha kufanya kazi katika net.
  11. Uwezo wa kutambua idadi nyingi ya vyombo vilivyounganishwa ndani ya kumpyuta.
  12. kuwepo kwa picha nyingi zenye kuvutia kwa ajili ya kupamba skirini (Backgrounds).
  13.  
KUANZA KUTUMIA WINDOWS:

Kabla ya kuanza kutumia windows unatakiwa kufanya mambo yafuatayo:-
1. Kuhakikisha waya wa umeme umeshaunganisha kwenye kompyuta yako. 2. Kufungua kompyuta kwa kutumia sehemu inayoitwa power. 3. Kusubiri mpaka idhihiri sehemu inayoitwa desktop.
Ndugu msomaji makala hii yenye anuani (hatua za kuendelea kompyuta imeletwa kwenu na ndugu Mahmoudu Twahiri Khamisi mwanafunzi wa chuo kikuu cha Al-zhar nchini Misr kitivo cha maktaba na teknolojia ya habari, naomba usome kwa makini na kama utakuwa unaujuzi zaidi nawe pia unatakiwa kuchangia ili tuweze kuwanufaisha ndugu zetu waswahili nao pia wafaidike na elimu ya kisasa, asanteni sana.


Ijue Computer ( Tarakilishi ). Sehemu ya II.

Tofauti ya Data na Habari.
Data: Ni ibara ya taarifa au maelezo, na inaweza kuonekana katika sura ya maandishi, michoro, picha, namba, alama, nembo, sauti au lugha ya maandishi, au sauti pamoja na picha.
Habari (Information):
Ni kazi inayotokana na taarifa au maelezo (Data) baada ya kwisha kupangiliwa na kufanyiwa kazi kisha kutoa matokeo kamili ya kazi hiyo, pamoja na kuleta kitu chenye kufahamika na chenye faida.

Sifa za kompyuta.

Wepesi: kompyuta inafanya kazi kwa wepesi wa hali ya juu kiasi kwamba unaweza kutafuta kitu kwa muda wa sekunde chache tu, kitu ambacho kama utakitafuta kupitia chombo chengine unaweza kuchukuwa wakati mrefu mpaka kukipata na pengine usikipate, kwa mfano unaweza kufanya hesabu ngumu kwa muda mchache kuliko kutumia akili yako. Pia unaweza kutafuta somo lolote kupitia internet kwa kutumia muda mfupi kulipata somo hilo kuliko ungetumia marejeo ya vitabu vya kuchapishwa.

Ubora:Kompyuta inafanya kazi kwa ubora zaidi bila kuonyesha udhaifu na makosa ya aina yoyote, na kama itabainika ya kwamba kuna makosa yametendeka kwenye kazi yako kompyuta kabla ya kuendelea kufanya kazi inakuonyesha kwamba upo katika makosa na kukutaka mara moja kurekebisha makosa hayo kwa kukuletea tangazo lenye sehemu kadhaa za kuchagua, ima kuendelea na kazi yako kama ilivyo au kufanya marekebisho ya kazi yako, kwa mfano unapotafuta kitu kutoka kwenye kompyuta, kompyuta kabla ya kutekeleza amri hiyo inakuletea tangazo na kukuuliza ya kwamba ni kweli una uhakika wa kutaka kufuta kitu hicho au umefanya hivyo bila kukusudia? pia kompyuta imekuandalia kila kitu unachotaka kukifanya ndani yake kutegemea na malengo yako mwenyewe. Pia kompyuta inazingatiwa ni mwalimu au muelekezaji (Instructor), kwani inakuelekeza jinsi gani unaweza kufanya kazi yako kwa ukamilifu.pia ndani ya kompyuta kuna kitu kinachoitwa kisaidizi (help)mbacho kinatumika kwa ajili ya kufanya utafiti wa kitu fulani ili kufahamu matumizi na njia zake.
Uwezo mkubwa wa kuhifadhi vitu: Miongoni mwa mambo muhimu ndani ya kompyuta ni kupatikana sehemu kubwa ya kuhifadhia vitu kwa amani na bila kupotea vitu hivyo.


Aina za matumizi ya kompyuta.

 Kuna aina kuu tatu za kompyuta, nazo ni kama ifuatavyo:-


1. Kompyuta Dijitali: Ni kompyuta zinazotumika kwa ajili ya kufanyia hesabu pamoja na kazi za kutumia akili.

2. Kompyuta Analogu:Ni kompyuta zinazotumika kwa ajili ya kupokea taarifa (Data) kama zile za kusomea hali ya hewa, kupimia mishipa ya damu na kupimia kiwango cha chumvi kwenye maji.

3. Kompyuta Mahuluti (Hybrid Computers):Kompyuta hizi zinafanana na zile zilizotangulia kutajwa hapo mwanzo, nazo zinatumika kwa ajili ya kutafutia taarifa (Data) kutoka kwa binadamu moja kwa moja na kupitia mandishi na vipimo.

Aina za kompyuta za digitali.

 

Super Computers:Takriban zinapatikana sehemu zote duniani, na zinauwezo na nafasi kubwa ya kuhifadhi vitu vingi (Information) na zinatumika kwa ajili ya kazi za kijeshi na sehemu za ukaguzi, pia kompyuta hizi haziruhusiwi kuhamishwa nje ya nchi na kujua jinsi gani zinatumika. Na zinasifika kuwa na umbile la kati na kati, pia zina uwezo mkubwa na uwepesi wa hali ya juu.

Mainframe Computers:Nazo ni kompyuta zenye umbile kubwa, na zilianza kudhihiri kwake katika mwanzo wa miaka ya hamsini, nazinasifika kwa uwezo mkubwa wa kuhifadhi vitu na pia uwepesi wa hali ya juu.

Mini Computers:Aina hizi za kompyuta zilidhihiri katika kipindi cha miaka ya sitini.Ni kompyuta zenye umbile dogo kuliko zile zilizotangulia kutajwa,na ni bora kwa kuunganishia kompyuta nyengine zinazotumika viwandani na ndani ya nchi.

Micro Computers:Aina hii ya kompyuta inakusanya aina zifuatazo:-
Kompyuta za Kibinafsi(PCs) ambazo ni maalumu kwa ajili ya matumizi ya mtu mmoja tu. Home Computers, Portable Computers: Nazo ni kompyuta za kubeba mkononi, ambazo zimegawanyika katika aina zifuatazo:- 1. Laptop. 2. Notebook. 3. Palmtop.

Kazi za msingi zinazofanyika ndani ya kompyuta.

 

  1. Kazi za uingizaji (Input).
  2. Kazi za uwendeshaji au ufanyishaji (Proccessing).
  3. Kazi za utoaji (Output).
  4. Kazi za kuhifadhi (Storege).

Matumizi ya compyuta.


Elimu:Kutokana na kuendelea kwa elimu ya teknolojia imetusaidia sana kujifunza mambo mbali mbali kupitia kompyuta, ambapo unaweza kutumia kompyuta kwa ajili ya kuuliza maswali na kujibiwa kwa haraka tena kwa njia tofauti, pia unaweza kutumia kompyuta kwa ajili ya kufanya majadiliano ya kielimu, pia unaweza kuandaa vipindi mbali mbali vya masomo na kufundishia elimu tofauti. Pia unaweza kuonyeshea filamu zenye mafundisho mazuri, kama kuonyesha filamu zenye elimu ya jeografia na sayansi ya mifugo na kilimo, kuonyesha sehemu muhimu za nchi yetu, kuonyesha athari za nchi ambazo ndiyo sehemu kuu zinazotuletea fedha za kigeni katika nchi yetu, na kuonyesha picha za maendeleo katika sekta mbali mbali za nchi yetu, pia kuonyeshea mila na tamaduni za taifa letu la Tanzania na mataifa mengine mbali mbali duniani n.k.

Michezo:Kompyuta zimeandaliwa ndani yake programu mbali mbali zenye michezo tofauti, ambayo inaweza kutumika na watu mbali mbali kutofautiana na umri wao, na ambayo inajulikana kama moja ya kazi za kukuza kipaji na kuchangamsha akili, na ni sehemu moja wapo ya kuburudisha nafsi.

Ufundi:Kompyuta zinaweza kutumika kwa ajili ya kufanyia kazi za ufundi, kama kuchora ramani ya nyumba na mazingira ya nje ya nyumba, kutengenezea picha kwa kuibadilisha na kuiremba na kuifanya ionekane katika sura nyengine ambayo tofauti na ile ya asili.

Mawasiliano:Kompyuta inaweza kutumika kwa ajili ya kufanyia mawasiliano kupitia mtandao wa (Internet) ambao leo hii ndiyo umeshika nafasi kubwa sana ya mawasiliano kuliko kitu chengine ulimwenguni, kama kuwasiliana kwa kutumiana ujumbe wa barua pepe (E-mail) ambayo ni rahisi na inafika haraka kuliko barua za kupitia posta, pia kwa kutumia barua pepe hakuna haja ya kufikiria sehemu aliko mtu America au Asia au sehemu nyengine duniani, kuwasiliana kwa maneno ya maandishi (Chat), pia kuwasiliana kwa maneno ya sauti na kuonekana picha.

Usafirishaji:Kwa kutumia kompyuta unaweza kuendeshea kazi za usafirishaji katika vituo vikuu vya usafirishaji, kama usafiri wa ardhini (mabasi, metro na treni), usafiri wa majini (meli), na usafiri wa angani (ndege).

Matumizi ya kiwandani:Kama kuendeshea mashine viwandani kwa ajili ya kuzalisha bidhaa mbali mbali, kama kutengenezea magari, kuzalishia umeme na kutengenezea bidhaa nyengine za kawaida kama nguo mazulia n.k.

Matumizi ya benki:Kama ilivyokuwa ada na kawaida hivi sasa kutumia kompyuta kwa ajili ya kuendeshea kazi za benki,kwa ajili kurahisisha kazi za mahesabu.

Kufanyia matibabu:Kompyuta zimekuwa na matumizi makubwa na muhimu sana katika kufanyia uchunguzi na matibabu hospitalini, kama kuchunguza na kuelekeza dawa ya kutibu ugonjwa uliyoonekana, pia kupimia na kujaribia mimba na kutoa maelekezo kuhusiana na siku na tarehe ya kujifungua.

Kazi za kompyuta.

1. Kuhifadhi vitu (Data):Kama ilivyotanguliwa kusemwa hapo awali kuwa kompyuta ni chombo pekee chenye uwezo mkubwa wa kuhifadhi vitu, na mpaka hivi sasa bado hakijapatikana chombo chengine chenye uwezo mkubwa wa kuhifadhia vitu zaidi ya kompyuta.

2. kuonyeshea matokeo ya vitu (Data na Information):Kutokana na kuendelea elimu ya teknolojia imeweza kuturahisishia kazi zetu nyingi ambazo tulikuwa tunazifanya kupitia vyombo mbali mbali, na kila chombo kilikuwa na kazi yake maalumu, tofauti na kompyuta ambapo mtu anaweza kuanzisha au kutengeneza kitu na wakati huo huo anaweza kukionyesha kwa kutumia kompyuta yenyewe, yaani kuonyesha ufanisi na sura nzuri ya kitu kilichofanyika.


Ijue Computer ( Tarakilishi ). Sehemu ya I.

 

Maana ya kompyuta ( tarakirishi ).ni mashine au chombo cha kielektroniki chenye uwezo wa kupokea na kukusanya taarifa (Data), kufanyia kazi na kutoa matokea ya kazi hiyo na namna ilivyoendeshwa, pamoja na kutoa matokeo ya kitu kilichofanyika, yaani kinachoonekana (Information)kwa haraka .

Tarakilishi ( computer. ).ni mashine inayotumia data kwa njia tofauti kutokana na maagizo zilizoandikwa kwenye bidhaa pepe (kwa Kiingereza software).

Maneno Kompyuta na Ngamizi yanaweza kutumika badala Tarakishi.
Teknolojia hii ni mabadiliko ya kisayansi yaliyowekwa kwenye nadharia ya utendaji kazi. Mabadiliko hayo yanapochochewa kwa kiasi kikubwa huwezesha mambo mbalimbali kuvumbuliwa na kuweza kuboresha shughuli mbalimbali za kijamii, kiuchumi na hata mawasiliano.
Kompyuta ni moja kati ya nyenzo zilizotokana na mabadiliko ya teknolojia ya hali ya juu.

HATUA KABLA YA MWANZO WA KOMPYUTA (1642).Msomi mmoja kutoka Ufaransa aliyekuwa anaitwa Pascal, alianzisha chombo cha kufanyia hesabu, ambacho alikitengeneza kwa ajili ya kumsaidia baba yake katika kazi za hesabu, lakini hakikuwa na sifa bora kama ilivyotakiwa. Kisha baada ya hapo kiliendelezwa na msomi mwengine kutoka Ujerumani, ambaye alijulikana kwa jina la Lebnitz na kuzidishwa ubora zaidi, kikawa kinafanya kazi zote za hesabu, kama vile kujumlisha, kutoa, kugawanya na kuzidisha, badala ya kufanya kazi za kuzidisha na kugawanya tu. Kisha msomi mwengine kutoka Uingereza alikuja kuanzisha chombo chengine cha hesabu, ambacho kilikuwa na uwezo mkubwa wa kuhifadhi vitu. Chombo hicho kilikuwa na sehemu kuu tatu, ambazo sehemu ya kwanza ilikuwa ni kwa ajili ya kuhifadhia kumbukumbu, sehemu ya pili ilikuwa ni kwa ajili ya kufanyia hesabu, na sehemu ya tatu na ya mwisho ilikuwa ni kwa ajili ya kuchapishia.


HATUA YA MWANZO (1944.)Kipindi cha mwaka 1944 kinajulikana kuwa ni mwanzo wa kudhihiri kompyuta. Kompyuta katika kipindi hicho ilikuwa ina sura tofauti na hivi sasa, kwani ilikuwa ni kubwa mfano wa chumba, na ilikuwa inatumika kwa ajili ya kufanyia hesabu tu, na ilikuwa inajulikana kwa jina la (ENIAC) Electronic Numerical and Calculation. Na mwisho wa mwaka 1951 ilianzishwa kompyuta nyingine ambayo ilikuwa inaitwa Unifac, na ilitengenezwa kwa ajili ya kufanyia biashara, na ilikuwa ni chombo pekee ambacho kilikuwa na uwezo mkubwa wa kuhifadhi vitu.

 

HATUA YA PILI (1958).

Kipindi cha mwaka 1958 kilifanikiwa kuendeleza chombo cha kompyuta, ambapo kilianzishwa chombo kinachoitwa Transistor, ambacho kiliwezesha kutengeneza kompyuta yenye umbo dogo baada ya kuwa na umbo kubwa mfano wa chumba. Vile vile chombo cha Transistor kiliwasaidia watumiaji wa kompyuta kipindi hicho kuepukana na joto kali lililokuwa linatoka kwenye kompyuta hiyo na kufanya kazi kwa ufanisi zaidi. Na mwanzo wa miaka ya sitini shirika la IBM lilianzisha chombo chengine cha kompyuta ambacho kilikuwa na maendeleo zaidi katika kipindi hicho.

 

HATUA YA TATU (1964).Kipindi hichi kilileta maendeleo makubwa sana katika kompyuta, ambapo chombo cha kompyuta kilitengenezwa kwa kutumia (Integrated Circuits) chombo hicho kilichukua nafasi ya Transistor. Na pamoja na maendeleo makubwa kutokea mwaka 1972 shirika la Intel lilifanikiwa kutengeneza Processor ndogo ambayo ilibadilisha sura nzima ya kompyuta katika umbo dogo sana (Mini Computer). Na hiyo ilikuwa ni sifa pekee ya mabadiliko makubwa ya kompyuta, na katika kipindi cha mwaka 1975 shirika la IBM lilianzisha kompyuta ya kutumiya mtu mmoja (Personal Computer), vile vile katika kipindi hicho zilianzishwa programu za kuendeshea vifaa vya kompyuta, na miongoni mwa programu hizo ilikuwepo programu ya (Dos) Disk Operating System, Application Programs, na programu za kutengeneza picha (Graphics).

 

HATUA YA NNE (1982).Mwanzoni mwa miaka ya themanini kulianza kuenea matumizi ya kumputa zenye kutumia Hard disk, na Processor zenye umbo dogo (Micro Processors) pamoja na programu za kuendeshea kompyuta (Operating System). Pia zilianzishwa kopi za programu za kuendeshea kompyuta (Dos), na hapo ndipo ilikuwa mwanzo wa kutumia windozi (Windows), na pia zilitumika programu nyingine ndani ya Windozi kama vile Word, Word 2, Word 6, Excel na power Point.

 

HATUA BAADA YA HATUA YA NNE. Kitu kinachosifika sana katika kipindi hichi ni kudhihiri kwa programu za Windozi na kuwa kama ni mazingira pekee ya kuendeshea kompyuta, na inajulikana wazi kwamba windozi ni kiini cha uendeshaji katika kazi za kompyuta, na imeitwa windozi kwa sababu unaweza kuitumia kufanyia kazi nyingi kwa wakati mmoja kwenye madilisha tofauti, kwa mfano pale mtumiaji anapokuwa anasubiri windozi moja ifunguke anaweza kuwa anasoma au kufanya kazi nyingine kwenye windozi nyingine pia.. Na windozi ya kwanza kudhihiri ilikuwa ni Windows 95, 98, 2000, Millennium kisha Windows XP, vili vile zilianzishwa programu maalumu kutoka kwenye shirika la Microsoft, kama vile Microsoft Office 97, Microsoft Office 2000 na Microsoft Office 2003, ambazo ambazo zinakusanya ndani yake Microsoft Word, Excel, Access na Power Point, pia zinajulikana kwa jina la application programs. Kisha kiliendelezwa kifaa cha Processor kutoka Pentium kwenda Pentium 2, Pentium 3 na Pentium 4, pamoja na kuzidi uwepesi wa kufikia vitu mpaka Giga Byte 2. Pia ilizidishwa nafasi ya kuhifadhia data ndani ya Hard disk kiasi cha kufikia Giga Byte 300, na kufikia nafasi ya Ram zaidi ya Mega Byte 512.

 

Historia ya magari.

Gari ya kwanza kabisa aina ya Benz 1885.
Motokaa. (kutoka Kiingereza "motor car", mara nyingi huitwa tu gari) ni chombo cha usafiri kinachotembea kwenye nchi kavu kikitumia nguvu ya injini au mota yake.
Kuna aina nyingi za motokaa; magari madogo hubeba abiria tu na gari dogo la kawaida hubeba dereva pamoja na abiria hadi wanne. Magari makubwa kidogo hubeba hadi watu 8.
Mengine ya kubeba abiria ni mabasi ambayo ni pia aina ya motokaa lakini mara nyingi hutajwa kama kundi la pekee, sawa na malori ambayo ni motokaa kubwa za kubeba mizigo. Kuna kila aina ya mchanganyiko kati ya aina hizi.

Muundo.

Motokaa huwa na injini (mota) inayosukuma magurudumu kupitia giaboksi. Injini pamoja na magurudumu na bodi hushikwa na fremu ya gari. Magari madogo ya kisasa huwa na bodi inayojibeba yenyewe bila fremu ya pekee. Motokaa nyingi huwa na magurudumu manne lakini magari mazito sana kama lori au basi mara nyingi huwa na magurudumu ya ziada.
Dereva hutumia mitambo ya kutawala motokaa ambayo ni hasa:
  • usukani wa kuongoza mwendo na mwelekeo wa gari
  • kichapuzi cha kutawala mbio au kasi yake
  • breki inayosimamisha chombo
  • mara nyingi pia mkono wa kubadilisha gia.
Mitambo ya lazima kwa usalama wa gari ni taa zake za nje mbele na nyuma, kiashirio au indiketa ya kuonyesha nia ya kubadilisha mwelekeo, kifuto au waipa inayosafisha kioo cha mbele wakati wa mvua.
Magari ya kisasa huwa na mitambo mengi mengine kama redio, vyombo vya muziki, kiyoyozi, siku hizi pia kompyuta ndogo ya kusimamisha injini au kuonyesha ramani ya njia pamoja na kutoa maelezo kuhusu njia kwa dereva kwa kutumia sauti iliyorekodiwa.
Injini kwa kawaida hupata nguvu yake kwa kuchoma petroli, diseli au gesi. Motokaa za kwanza zilitumia pia nguvu ya mvuke. Motokaa za kisasa kabisa zinatumia pia injini ya umeme.

  

Historia ya motokaa.

Kwa karne nyingi watu walitumia magari yaliyovutwa na wanyama kwa mfano farasi, punda au maksai. Waroma wa kale walifanya majaribio na magari yaliyosukumwa na watumwa. Maendeleo ya uhandisi yalisababisha majaribio ya kutengeneza magari yaliyosogezwa kwa nguvu ya upepo yakitumia tanga kuanzia mwaka 1600 huko Uholanzi.


Injini za mvuke.Baada ya kugunduliwa kwa injini ya mvuke nguvu yake ilitumiwa pia kwa vyombo vya usafiri. Kutokana na uzito wa injini pamoja na magari yaliyoweza kuvumilia uzito mkubwa wa injini pamoja na maji na kuni iliyohitajika kuchemsha maji vyombo hivi havikufaa barabara za kawaida vikatumia njia ya reli za chuma. Nusu ya pili ya karne ya 19 iliona maendeleao ya kutengenezwa kwa motokaa za mvuke madogo yaliyotembea barabara za kawaida katika nchi za Ulaya na Marekani.

 

Injini za umeme.

Sehemu ya pili ya karne ya 19 iliona pia magari yaliyoendeshwa kwa nguvu ya umeme. Magari haya yana faida nyingi; muundo wa gari ni rahisi zaidi kwa sababu haihitaji giaboksi wala gia na gari halina makelele pia hautoi herufu baya ya eksozi. Lakini magari haya yalikuwa na tatizo ya kwamba yalitegemea kupata nichati kwa njia ya beteri nzito zilizochukua muda mrefu kuchajiwa. Hata hivyo hadi mwanzo wa karne ya 20 magari ya umeme yalikuwa mengi katika miji mikubwa.


Basi ya umeme mjini San Francisco inapokea nishati kupitia waya juu ya barabara inapopita
Mwaka 1900 asilimia 40 za motokaa zote nchini Marekani zilikuwa na injini za mvuke, 38 % za umeme na 22% za petroli. Mjini New York nusu ya motokaa zote zilikuwa na injini ya umeme.
Baadaye magari ya petroli yalisogea mbele kwa sababu yaliweza kutembea mbali kwa kujaza mafuta kuliko gari la umeme kwa beteri yake tena beteri ilichua masaa hadi kujazwa upya wakati mafuta hujazwa mara moja.
Katika nchi kadhaa mabasi ya umeme yameendelea kutumiwa katika miji mikubwa yakipokes nishati si kwa beteri bali kwa nyaya za umeme zinazopangwa juu ya barabara ambako basi inapita.


Injini za mwako ndani.

Injini mwako ndani imekuwa hadi leo njia kuu ya kusogeza magari na kwa kawaida tukiongelea motokaa tunamaanisha gari lenye injini mwako ndani inayochoma petroli au diseli.
Katika karne ya 19 wahandisi mbalimbali walianza kutengeneza injini za mwako wa ndani zilizochoma gesi au petroli ndani yake. Injini ya kwanza iliyofaulu kuanzia 1876 na kutengenezwa kwa wingi ilikuwa ni ile ya Mjerumani Nikolaus Otto aliyeshirikiana na Gottlieb Daimler na Wilhelm Maybach. Ilikuwa na mapigo manne petroli ikichomwa kwa msaada wa mwasho wa umeme na hadi leo sehemu kubwa ya injini zote inafuata kielelezo wa Otto. 1879 Karl Benz alitengeneza injini ya mapigo mawili kwa mfano wa Otto akaitumia kwa gari lake na tangu 1885 akatoa aina ya kwanza ya motokaa yenye magurudumu matatu iliyoendelea kujengwa mfululizo yaani kibiashara.
Maendeleo ya motokaa zilizotumia injini mwako ndani yalikuwa haraka. Mwanzoni yalikuwa na matatizo mengi hasa uhaba wa petroli. Benz alinunua mafuta kwa gari lake kwenye duka la dawa.
1892 mhandisi Mjerumani Rudolf Diesel alitunga injini inayochoma mafuta kwa kuikandamiza vikali na kutumia joto la hewa ndani ya injini kutokana na mshtuko wa kukandamizwa. Mashine hizi zina uwezo kutumia aina mbalimbali za mafuta na ile ya kawaida ilikuwa nzito kuliko petroli ikaitwa "diseli". Injini za diseli zamani hazikupendwa kwa magari madogo kutokana na sauti kubwa zaidi ya injini lakini zikawa kawaida kwa malori, mabasi na injini za meli kwa sababu zinatumia mafuta kidogo kuliko injini za petroli.


Ushindi wa motokaa.

Mwanzoni motokaa zilikuwa ghali sana zikanunuliwa na matajiri pekee. Mwaka 1914 mhandisi wa Marikani Henry Ford alianza kutengeneza gari lake la "Ford Model T" kiwandani akitumia mbinu mpya; aligawa matengenezo ya gari kwa hatua mbalimbali zilizotekelezwa na wafanyakazi walioshughulika hatua moja-moja tu. Mbinu huu ulisababisha utekelezaji wa haraka kwa sababu kila mfanyakazi alikuwa na shughuli chache zu alizojua kwa undani kabisa akiwa na vifaa na vipuri vyote pale alipofanya kazi bila kupotezy muda. Kwa njia hii Ford aliweza kutengeneza magari mengi tena kwa bei nafuu na hata watu wenye mapato ya wastani waliweza kununua gari hili. Mfanyakazi wa Ford aliweza kununua gari kwa mshahara wa miezi minne. Kwa jumla magari milioni 15 ya Ford T yalitengenezwa hadi 1927.
Wengine waliiga mfano wa Ford na motokaa zilizidi kupanua. Baada ya vita kuu ya pili ya dunia polepole katika nchi nyingi za Ulaya, Amerika na Asia motokaa ilikuwa njia ya kawaida ya usafiri kwa watu wengi.
Upanuzi wa usafiri wa motokaa ulibadilisha tabia nyingi za nchi zilizoathiriwa nao. Miji ilibadilika kwa kutengeneza barabara pana za kupokea magari mengi. Watu walianza kuishi mbali na mahali pa kazi kwa sababu usafiri ulikuwa rahisi na haraka. Njaa ya petroli na diseli iliendelea kuzidi na nchi zenye akiba za mafuta ya petroli zilitajirika kwa mfano nchi za Uarabuni, Norwei au Venezuela.


Mielekeo mipya.

Tangu miaka ya 1970 kuzidi kwa motokaa kulileta pia matizo mapya:
  • machafuko kwa mazingira kwa kelele na hewa chafu ya eksozi. Machafuko haya yalionekana kusababisha magonjwa kama kansa pia kuleta uharibifu kwa machafuko kwa hewa. Matokeo yake yalikuwa mvua asidi inayohatarisha mimea pamoja na misitu, wanyama ndani ya maziwa na pia kuharibu majengo hasa majengo ya kihistoria.
  • kupanda kwa bei ya petroli tangu vita ya Oktoba 1973 kati ya Waarabu na Israeli. Ilionekana mara ya kwanza ya kwamba nchi zenye mafuta zina uwezo wa kusumbua uchumi wa nchi wateja kwa kusimamisha utengenezaji.
  • hofu ya kuishi kwa mafuta ya petroli baada ya Klabu ya Roma kutoa taarifa yake ya kwanza iliyoeleza ya kwamba malighafi yote duniani yana mwisho na yatakwisha siku moja.
Jibu la wahandisi lilikuwa majaribio ya kuboresha injini zisizotumia mafuta. Ni hasa teknolojia mbili zilizoendelea kushughulikiwa:
  • injini ya gesi
  • injini ya umeme
Kwa jumla magari ya umeme bado hutegemea mbinu za kubeba nishati njiani kwa beteri. Siku hizi ni hasa injini za umeme zinazopokea jitihada nyingi. Tatizo hadi leo ni uzito, uwezo na gharama za beteri. Hata kama zimeshoboreka sana bado chaji ya beteri inaruhusu safari ya kilomita 50-100 tu. Kuchajiwa upya kunachukua masaa. Kuna mawazo ya kuunda mfumo wa vituo vya beteri ambako beteri zingebadilishwa sawa na vituo vya mafuta vya leo.
Mwelekeo tofauti ni majaribio ya kutengeneza umeme njiani. Hapa kuna njia mbili hasa:
  • Daimler-Benz na makampuni menine yametengeneza magari yenye teknolojia mpya ya seli ya fueli inayotumia haidrojeni. Lakini hadi sasa nguvu yake haitoshi kwa magari ya kawaida. Utafiti unaendelea.
  • hasa makampuni ya Japani yameshafaulu kutoa na kuuza magari chotara yanaounganisha injini ya umeme na injini ya petroli. Gari linaanza safari kwa nguvu ya beteri; beteri ikikwisha injini ya mafuta inawaka na kujaza beteri.

Thursday, July 18

Mipango ya Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia ya Taifa la China.


Mpango wa Utafiti wa Kimsingi
Mpango wa utafiti wa kimsingi ulianza kutekelezwa mwezi wa Machi mwaka 1997, mpango huo pia unaitwa mpango wa “973”.
Mpango wa “973” unahusu kilimo, nishati, upashanaji habari, maliasili, mazingira, idadi ya watu na afya na nyenzo.
Katika miaka ya karibuni, serikali imetenga fedha yuan milioni mia kadhaa kwa ajili ya mpango huo na imeanzisha miradi zaidi ya 300, na baadhi ya miradi iliyoanzishwa mapema imepata mafanikio.
Mpango wa Utafiti wa Sayansi na Teknolojia ya Juu
Mpango huo ulitolewa na wanasayansi wakubwa wanne wa China katika mwezi Machi mwaka 1986, kwa hiyo mpango huo pia unaitwa mpango wa “863”.
Mpango wa “863” umechagua miradi 15 ya utafiti wa viumbe, anga ya juu, upashanaji habari, laser, mfumo unaojiendesha, nishati, nyenzo mpya n.k.
Ili kutekeleza mpango huo wa “863” vituo vingi vya utafiti wa sayansi na teknolojia ya juu vimeanzishwa, na vimeandaa wanasayansi wengi vijana, mafanikio mengi yenye kiwango cha kimataifa yamepatikana.
Mpango wa Kuendeleza Sayansi na Teknolojia ya Kilimo
Mpango huo wa sayansi na teknolojia ya kilimo pia unaitwa “mpango wa cheche za moto”. Neno “cheche za moto” linatokana na usemi wa Kichina “cheche za moto zaweza kuunguza mbuga kubwa”, ikimaanisha kuwa sayansi na teknolojia ya kilimo vinaweza kuenea haraka kote nchini China.
Mpango huo ulianza kutekelezwa mwaka 1986. lengo la mpango huo ni kuvumbua teknolojia mpya ya kilimo na kuieneza vijijini na kuwaelimisha wakulima watumie teknolojia mpya kuendeleza kilimo.
Katika miaka zaidi ya kumi tokea mpango huo uanze kutekelezwa wataalamu wa kilimo wamevumbua teknolojia nyingi na kwa kiasi kikubwa wameendeleza kilimo. Mwaka 2003 wataalamu wa kilimo waliotesha aina zaidi 300 za mbegu bora na kutumika katika hekta milioni 10, na walitoa njia mpya ya umwagiliaji ambayo inaokoa maji kwa 30%.
“Mpango wa cheche za moto” umesukuma uzalishaji wa aina moja ya kilimo kwa kiwango kikubwa na wa kisasa, umeongeza mapato ya wakulima na kuwafahamisha kuwa teknolojia ndio mali. Watu wa nchi za nje wanasema “mpango wa cheche za moto” ni mpango wa kuwaendeleza wakulima.
Mpango wa kueneza matokeo ya teknolojia mpya za hali ya juu
“ Mpango wa mwenge” yaani mpango wa China wa kueneza matokeo ya teknolojia mpya za hali ya juu ni mpango wa kuelekeza katika kuendeleza shughuli za teknolojia mpya za hali ya juu. Mpango huu unalenga kuenzi nguvu bora za sayansi na teknolojia za China, kuhimiza matokeo ya teknolojia mpya za hali ya juu yatumiwe katika kuzalisha bidhaa na kuzifanya bidhaa hizo ziingie kwenye soko la nchini na duniani. Mpango huu ulitekelezwa kuanzia mwaka 1988. Sekta muhimu za kuendeleza teknolojia mpya za hali ya juu ni kama vile elektroniki na upashanaji habari, teknolojia za viumbe, nyenzo mpya, nishati mpya, kubana matumizi ya nishati na kujipatia ufanisi wa juu na kuhifadhi mazingira.
Hivi sasa China imeanzisha sehemu 53 za kitaifa za maendeleo ya teknolojia mpya za hali ya juu. Toka mwaka 1991 hadi hivi sasa, wastani wa ongezeko la malengo muhimu ya uchumi wa sehemu hizo unafikia asilimia 40 kwa mwaka. Sehemu hizo zimekuwa nguzo za kusukuma mbele maendeleo ya teknolojia mpya za hali ya juu na kuboresha miundo ya uchumi wa taifa.
Mwaka 2004, mapato ya sehemu 53 za maendeleo ya teknolojia mpya za hali ya juu yalizidi renminbi yuan trilioni 2, sehemu kadha wa kadha maarufu miongoni mwa sehemu hizo kama vile Sehemu ya sayansi na teknolojia ya Zhongguanchun ya Beijing na Sehemu ya teknolojia mpya ya hali ya juu ya Shanghai, mapato yao ya mwaka 2004 yalizidi yuan bilioni 150. Na katika sehemu hizo pia zimeanzishwa kwa mashirika mengi ya shughuli za teknolojia mpya za hali ya juu kama vile Kampuni ya kompyuta ya Lenovo, Kampuni ya kompyuta ya Fonder, makampuni ya upashanaji habari ya Huawei na Datang.
Mpango wa China wa chombo cha safari ya anga ya juu ya kubeba binadamu
Mpango huo umetekelezwa kuanzia mwaka 1992. Mpango huo unatekelezwa kwa hatua tatu, ya kwanza ni kuwapeleka wanaanga wa China kwenye anga ya juu; ya pili ni kutatua teknolojia husika ili kurusha maabara ya anga ya juu yenye watu ambayo itawekwa kwenye anga ya juu kwa muda mfupi; ya tatu ni kujenga kituo kinachotunzwa na watu kwa muda mrefu ili kutatua masuala ya kufanya majaribio makubwa ya kisayansi na teknolojia ya matumizi kwenye anga ya juu.
Mwishoni mwa mwaka 1999 China ilifanikiwa kurusha na kurudisha Chombo cha Shenzhou No.1cha safari za anga ya juu. Katika zaidi ya miaka mitatu baada ya hapo, China ilifanya majaribio mara tatu ya kurusha chombo cha safari ya anga ya juu bila kubeba binadamu. Tarehe 15 Oktoba mwaka 2003 China ilirusha Chombo cha Shenzhou No.5 kilichobeba binadamu kwenye safari ya anga juu, Bwana Yang Liwei amekuwa mwanaanga wa kwanza wa China kwenye anga ya juu. Kufanikiwa kurushwa kwa Chombo cha Shenzhou No.5 kumeonesha kuwa China imekuwa nchi ya tatu duniani ikiifuata Russia na Marekani kuwa na uwezo wa kuanzisha shughuli za kubeba binadamu kwenye safari ya anga ya juu kwa kujitegemea.
Roketi zilizotumiwa katika kurusha vyombo vya safari ya anga ya juu vya China zilisanifiwa na kutengenezwa kwa ajili ya vyombo vya kubeba binadamu kwenye safari ya anga ya juu. Roketi ya Changzheng No.2 F ni roketi kubwa kabisa, ndefu kabisa na yenye miundo mingi ya utatanishi kabisa.
Habari zinasema kuwa, mwaka 2006 China itarusha chombo cha safari ya anga ya juu ya Shenzhou No.6, ambapo chombo hicho kitawabeba wanaanga kadhaa, na wanaanga hao huenda wataweza kutoka kwenye chombo na kutembea kwenye anga ya juu.
Mradi wa China wa kufanya utafiti kwenye mwezi
Mradi huo utatekelezwa kwa vipindi vitatu: Kwanza, kurusha satlaiti itakayouzunguka mwezi na kufanya utafiti wa mwezi; Pili, kukifanya chombo cha utafiti wa mwezi kitue kwenye ardhi ya mwezi ili wanaanga waweze kutembea na kufanya uchunguzi kwenye ardhi ya mwezi; tatu kukamilisha kazi ya chombo kutembea na kufanya uchunguzi kwenye ardhi ya mwezi na kurudisha chombo kwenye dunia. Hivi sasa kazi ya kipindi cha kwanza inafanyika.
Mradi wa kurusha satlaiti ya itakayouzunguka mwezi na kufanya utafiti umetekelezwa kuanzia mwezi Januari mwaka 2004, China itarusha satlaiti ya Chang'e No.1 kwa kufanya utafiti kwenye ardhi ya mwezi.
China imeendeleza shughuli za safari ya anga ya juu katika zaidi ya miaka 40 iliyopita, na imekuwa na uwezo wa kusanifu na kutengeneza yenyewe rekodi za uchukuzi na satlaiti, tena imesanifu na kutengeneza chombo cha safari ya anga ya juu, mwaka 2004 ilifanikiwa kurusha chombo cha kubeba mwanaanga kwenye safari ya anga ya juu. Lakini wanasayansi wa China wanaona kuwa, bado kuna matatizo mengi ya kiteknolojia katika kufanya utafiti wa mwezi.
Habari zinasema kuwa, hivi sasa China inafanya ukarabati wa mfumo wa upimaji na udhibiti wa upashanaji wa habari na mfumo wa ardhini katika mradi wa kurusha satlaiti ya China itakayorushwa ili kuuzunguka mwezi na kufanya utafiti wa mwezi, na kazi ya kusanifu na kutengeneza satlaiti na mfumo wa roketi kabla ya mwezi Oktoba mwaka 2006.

Maelezo kuhusu Sayansi na Teknolojia kwa Ufupi.

Katika miaka ya karibuni China imekuwa ikitekeleza mkakati wa “kuimarisha taifa kwa sayansi na elimu”, inatilia maanani sana maendeleo ya sayansi na teknolojia na imeongeza fedha katika utafiti wa sayansi na maendeleo ya teknolojia. Mwaka 2003 fedha zilizotumika katika utafiti wa sayansi na maendeleo ya teknolojia zilizidi yuan bilioni 150, ambazo ni 1.35% ya pato yote la taifa.
Hivi sasa mpango wa kuendeleza sayansi na teknolojia unatekelezwa katika sekta ya utafiti wa kimsingi, sayansi na teknolojia ya juu, kilimo, maendeleo ya mashirika ya teknolojia ya kisasa, teknolojia ya anga ya juu na ulinzi wa taifa. Serikali inachagua mashirika kutekeleza mpango huo kwa kufanya zabuni na kutenga fedha za utafiti kwa mashirika hayo.
Kutokana na juhudi za miaka mingi, China imekuwa na uwezo wa utafiti wa sayansi na uvumbuzi wa teknolojia mpya, mafanikio ya utafiti yamefikia au yamekaribia kufikia kiwango cha kisasa cha kimataifa. Mwaka 2003 tasnifu zilizotolewa na wanasayansi wa China zilichukua nafasi ya tano duniani, na hakimiliki za uvumbuzi pia ziliongezeka kwa kiasi kikubwa.

Wednesday, July 17

Mfumo wa jua na sayari zake.

Mfumo wa jua na sayari zake: ni utaratibu wa jua letu na sayari au sayari kibete zinazolizunguka pamoja na miezi yao, asteroidi, meteoridi, kometi na vumbi ya angani yote ikishikwa na mvutano wa jua.
Kwa kawaida huhesabiwa sayari 9 zinazozunguka jua. Lakini miaka ya nyuma magimba makubwa yamegunduliwa angani ambayo bado hayakukubaliwa kama yahesabiwe kuwa sayari au aina ya asteoridi.
Orodha inayofuata bado inahitaji kuangaliwa kwa sababu kuna tofauti kati ya kamusi na vitabu mbalimbali jinsi ya kutaja sayari fulani.

 Sayari za jua letu: Sayari katika mfumo wa jua ni zifuatazo:
Namba zote zinazotaja sifa mbalimbali za sayari zinaonyesha kipimo kulingana na tabia za dunia yetu kuwa "1". Kuhusu majina ya sayari kadhaa kuna mchanganyiko katika kamusi na vitabu. Pale ambako jina au umbo tofauti la jina ni kawaida linaonyeshwa katika mabano kama (jina). Majina yanayotumiwa katika vitabu kadhaa bila kuwa na uhakika yanaonyeshwa katika mabano ya italiki pamoja na alama ya swali kama (? jina).

Utaridi ni jina la sayari ya kwanza kutokana na lugha ya Kiarabu. Vitabu vingine hutumia neno "Zebaki" ni pia neno lenye asili ya Kiarabu linalomaanisha metali; inaonekana limepatikana kama tafsiri ya jina la Kiingereza la sayari ya kwanza "Mercury" bila kujua historia ya majina ya sayari sita ya kwanza yaliyoingia katika Kiswahili kutoka lugha ya Kiarabu.
** Zuhura - Ng'andu ni sayari lenye jina la Kibantu kwa Kiswahili pamoja na jina la asili ya Kiarabu
*** Tazama makala ya Dunia kwa ajili ya namba halisi. Neno "ardhi" hutumika na waandishi kadhaa badala ya "dunia" wakitaka kutaja sayari ya tatu.
**** Tangu 2006 Pluto imeingizwa katika kundi la "sayari kibete".

Mwezi (gimba la angani)

Sayari inaweza kuwa bila mwezi au na miezi mingi. Dunia yetu ina mwezi moja tu. Mshtarii ina miezi zaidi ya 60, mingine mikubwa kama sayari ndogo mingine midogo yenye kipenyo cha 1 km tu. Utaridi haina mwezi.
Mwezi hauna nuru mwenyewe bali kunang'aa jwake kunatokana na nuru ya jua inaoakisiwa usoni mwake kama kwenye kioo.

Mwezi wa Dunia (ardhi) yetu

Mwezi wa dunia yetu ni mkubwa kushinda miezi mingine katika mfumo wa jua. Hakuna jina tofauti kuliko "mwezi" isipokuwa watu wametumia neno la Kilatini "luna" kwa ajili ya mwezi wakitaja mwezi wetu ili kuutofautihsa na miezi ya sayari nyingine.
Huwa tunaangalia uso wake upande mmoja tene uleule tu. Sababu yake ni ya kwamba siku ya mwezi ni sawa na kipindi cha mwezi duniani. Mwezi unazunguka kwenye kipenyo chake katika muda wa siku 27.321 661 za dunia. Upande wa nyuma wa mwezi uko gizani wakati sisi tunaona mwezi mpevu. Wakati kwetu mwezi hauonekani upande wa nyuma unapokea nuru ya jua.
Uso wa mwezi unajaa mashimo ya kasoko yaliyosababishwa kwa kugongwa na meteoridi. Mwezi hauna angahewa inayozuia mapigo ya meteoridi ndogo au kupunguzu nguvu yao jinsi ilivyo duniani.


Mwezi (wakati) kama kipimo cha wakati

Awamu za mwezi kuanzia mwezi mwandamu kupitia robo ya kwanza, nusu mwezi, mwezi mpevu, robo ya tatu hadi mwezi mwandamu tena
Uso wa mwezi jinsi unavyoonekana duniani hubadilikabadilika. Mwezi mpevu unaonekana kama duara kamili la kung'aa lakini baada ya kuonekana hivi umbo lapungua kila siku hadi kutoonekana kabisa na hali hii huitwa mwezi mwandamu. Baadaye mwezi unaonekana tena kama hilali nyembamba na kuongezeka hadi kuwa duara tena. Muda wa mabadiliko yote kupit mara 1 ni siku 29 1/4.
Muda wa mabadiliko kati ya mwezi mwandamu hadi kupotea na kuwa mwezi mwandamu tena ni kati ya siku 28 - 29. Kipindi hiki kinakumbukwa kirahisi, kinatazamiwa na watu wote wakati uleule kwa hiyo pamoja na kipindi cha siku kilikuwa kati ya vipimo vya kwanza vya wakati kwa binadamu.
Awamu za mwezi zilikuwa vipindi vya kuhesabu wakati tangu mwanzo wa kalenda. Hadi leo kuna kalenda ya mwezi ndiyo kalenda ya Kiislamu inayopanga wakati kutokana na hali halisi ya awamu za mwezi.

Safari kwenda mwezini


Nyayo za mwanaanga Edwin Aldrin mwezini  (Apollo 11)
Mwezi wetu ni gimba la anga la kwanza ambako wanadamamu wamefika. Tarehe 21 Julai 1969 mwanaanga Mwamerika Neil Armstrong alikuwa mtu wa kwanza wa kukanyaga uso wa mwezi. Waamerika 11 walimfuata katika miaka hadi mwaka 1972. Baadaye safari za kwenda mwezini hazikufanywa tena kutokana na gharama kubwa.

Mwezi mali ya watu?

Hata kama Warusi na Waamerika walifikisha mabendera yao mwezini hakuna anayedai mali huko. Katika mkataba wa kimataifa kuhusu anga wa nje nchi 192 za dunia zimepatana ya kwamba mwezi utaangaliwa sawa na maeneo ya kimataifa ya bahari. Walipatana pia ya kwamba itakuwa marufuku kupeleka silaha kali kama kinyuklia angani. Mataifa mengi ya dunia yamejiunga na mkataba huo isipokuwa nchi chache hasa za Afrika hazikutia sahihi kama vile Tanzania.
Lakini kuna watu binafsi wanaodai mali ya mwezi. Kwanza kuna familia ya Jürgens wanaoishi Westerkappeln (Ujerumani) walipewa hati ya kumiliki mwezi na mfalme wa Prussia Friederich II. tarehe 15.07. 1756 BK. Mfalme alitoa hati kama zawadi ya shukrani kwa huduma bora akiamuru ya kwamba Martin Jürgens atakuwa mwenye mwezi na haki hii itarithiwa na mtoto wa kwanza.
Bila shaka ilhali hakujua haki za mali za Mjerumani katika mwaka 1980 Mwamerika Dennis M. Hope alifika mbele ya msajili wa viwanda mjini San Francisco akidai mwezi ni wake. Kufuatana na sheria ya Marekani kiwanda ni mali ya mtu akiandikisha dai lake na katika muda wa miaka minane hakuna upingamizi dhidi ya dai lake. Kwa njia hii -iliyowahi kufaulu tayari wakati wa karne zilizopita Wazungu walipojipata Amerika ya Kaskazini (hakuna aliyepinga madai yao mbele ya msajili)- alipata hati ya kumiliki akijaribu kuuza sasa mwezi polepole.

Je! unamjua Neil Armstrong?

Mwanaanga:Alizaliwa katika familia ya wakulima kwenye jimbo la Ohio tarehe 5 Agosti 1930. Baada ya kumaliza shule alijiunga na jeshi ambako alipata mafunzo ya uhandisi na kuwa rubani. 1952 alishiriki katika vita vya Korea.

Rubani wa majaribio:Mnamo mwaka 1955 aliajiriwa na taasisi ya mambo (shughuli za) (utafiti wa mambo) ya anga (NASA) kama rubani wa majaribio kwa aina mpya za ndege. Mnamo mwaka 1958 alikuwa mmojawapo katika kundi la marubani waliotayarishwa kupelekwa angani.

Mwanaanga:Baada ya kuundwa kwa NASA aliingia katika kundi la wanaanga. Safari yake ya kwanza ilikuwa 16 Machi 1966 kama mwanaanga kiongozi wa Gemini 8. Kilele cha safari hii ilikuwa kukutana kwa Gemini 8 na satelaiti nyingine na kuunganisha vyombo vyote viwili kwa muda wa masaa kadhaa.

 Safari ya kwenda mwezini:Baadaye aliteuliwa kuwa makamu wa kikundi cha wanaanga waliokwenda mwezini kwa kutumia chombo kilichoitwa Apollo 11. Ajali ya Apollo 1 iliyosababisha kifo cha mwenzake hapo kabla, ndiyo iliyompelekea kujiunga kwake na kundi la Apollo 11. Tar. 20 Julai 1969 Neil Armstrong pamoja Edwin Aldrin waliutataga uso wa mwezi wakiwa wanadamu wa kwanza mwezini. Walitoka katika chombo cha angani na kutembea mwezini kwa mara ya kwanza. Picha hizi zilionyeshwa kote duniani. Akiwa katika hali hii, Armstrong alitamka maneno yafuatayo: "Hii ni hatua ndogo kwa mtu lakini hatua kubwa kwa ubinadamu."

Baada ya kurudi salama, Armstrong aliacha kazi katika NASA na badala yake akawa profesa wa uwanaanga kwenye chuo kikuu cha Cincinnati katika mwaka 1971 hadi alipostaafu na kujishugulisha na biashara zake.

Waturuki wai 'HACK' website ya microsoft.

Kundi la vijana wa kituruki limekuwa likishindana na kundi la vijana wengine wa Urusi katika kuziteka tovuti mbali mbali duniani.

Mwaka 2005 kundi hilo lilifanikiwa kuziteka computer za vyombo vikubwa vya habari vya marekani kama vile CNN, New York Times, ABD News na vinginevyo na kufanikiwa kutuma virusi kibao ambavyo vilivuruga mitambo yao.

Mojawapo ya tovuti zilizowahi kutekwa na kundi la waturuki ni tovuti ya aliyekuwa mgombea wa nafasi ya uraisi wa Marekani kupitia chama cha Republican Duncan Hunter,tovuti ya chama cha soka cha Denmark ,tovuti ya NGO moja ya kupambana na ukimwi nchini Ufaransa ya Solydays.

Katika tukio la jana vijana hao waliwashangaza wadau wa Microsoft waliotembelea tovuti hiyo jumanne asubuhi kwa kukuta meseji ya EID MUBARAK na meseji yao ya kujipongeza kwa kuiteka website hiyo.

Hata hivyo wataalamu wa microsoft walifanikiwa kurekebisha tatizo hilo ingawa liliwachukua masaa kadhaa.

Msemaji wa Microsoft Ireland alisema "Hakukuwa na ubadhirifu wowote uliofanyika kutokana na tukio hilo".

"Kulikuwa na mapungufu katika ulinzi wa tovuti yatu ,Wataalamu wetu wanashughulikia tatizo hili ili lisitokee tena " aliongeza msemaji huyo.


Chanzo: NIFAHAMISHE

Serikali yatenga bil. 30 kwa tafiti za kisayansi.

Serikali  imewekeza Sh.bilioni 30 kwa ajili ya utafiti wa kisayansi kwa wanafunzi wa shule mbalimbali za sekondari hususani wale wanaosomea masomo hayo.
Hayo yalisemwa na Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa wakati wa kukabidhi zawadi kwa wanafunzi wa shule zilizoshinda shindano la kutafuta wanasayansi chipukizi toka shule 100 nchini.
“Bila kuwekeza katika utafiti wa kisayansi, nchi haiwezi kuendelea…hivyo kama serikali tumeamua kutenga kiasi hicho kwa lengo la kufanyia tafiti mbalimbali kuanzia kwa wanafunzi hawa toka shule mbalimbali hapa nchini,” alisema Profesa Mbarawa.
Profesa Mbarawa alisema serikali itaboresha utafiti huo ili kuwapa nafasi wanafunzi wengi kuwa wagunduzi wa mambo ya kisayansi kutokana na sayansi kutokuwa na mipaka.
Alisema ili kuendeleza sayansi nchini, serikali imejenga chuo kikubwa kiitwacho Nelson Mandela jijini Arusha na kutarajiwa kuzinduliwa Novemba 2, mwaka huu, chenye lengo la kuendeleza utafiti wa sayansi.
Aidha, alisema katika mashindano ya wanasayansi chipukizi toka shule mbalimbali za sekondari nchini, serikali itawasaidia waandaji wake, Young Scientists Tanzania  (YST), kuwezesha wanafunzi zaidi kushiriki tofauti na sasa ambapo shule 100 zenye wanafunzi 300 hushiriki.
“Taasisi nyingi nazo za tafiti za kisayansi zinatakiwa kushiriki maonyesho kama haya siku zijazo…lengo letu likiwa ni kuwekeza katika sayansi nchini,” alisema.
Awali mkurugenzi wa YST, Gosbert Kamugisha alisema lengo la mashindano hayo kwa wanasayansi chipukizi toka shule mbalimbali za sekondari nchini, ni kulenga tafiti za kisayansi.
“Wanafunzi walitakiwa kuandika maombi ya kisayansi yenye kulenga tafiti za kisayansi…tumeshirikisha wanafunzi 300 toka shule 100 za Bara na Visiwani, na washindi wametangazwa na kupewa zawadi zao,” alisema Kamugisha.
Alisema katika mashindano hayo watafiti wa kisayansi toka Chuo cha Taifa cha Ireland, walikuwa wakitoa muongozo.
Katika mashindano hayo, shule ya wasichana ya Kibosho ya Moshi mkoani Kilimanjaro, ilifanikiwa kushika nafasi ya kwanza na kujishindia nishani, Sh.Milioni moja pamoja na kompyuta mpakato (Laptop) tatu.
Wizara ilitoa Laptop hizo kwa wanafunzi watatu wa shule hiyo wanaosoma kidato cha tano waliofanya vizuri ambao ni Monica Shirika na Nengai Moses wanaochukua mchepuo wa PCB pamoja na Aisha Nduka wa mchepuo wa PCM, huku shule ya Ilboro Arusha ikikabidhiwa Sh.Milioni Moja kwa ushindi wa pili.

TANZGLO