WAAFRIKA na imani za kishirikina ni kama mapacha. Inaonekana kwa baadhi ya Waafrika kuacha imani za kishirikina ni jambo ambalo haliwezekani kwani hali hiyo imejitokeza katika Fainali za Afrika zinazoendelea nchini Afrika Kusini.
Mashabiki wa Ghana, DR Congo na Niger wanapanga
kupeleka malalamiko yao kwa waandaaji wa Fainali za Afrika 2013 ili
kuwazuia wanawake wasiwasogelee wachezaji wao kwenye Uwanja wa Nelson
Mandela Bay zinazoutumia uwanja huo.
Tayari mashabiki hao wameishawafuata walinzi wa
uwanja huo na
kuwaambia wasikubali wanawake kukaribia vyumba vya kubadirishia nguo wachezaji.
kuwaambia wasikubali wanawake kukaribia vyumba vya kubadirishia nguo wachezaji.
“Tumeambiwa tuwazuie wanawake kukaribia vyumba vya
kubadilishia nguo wachezaji kwa sababu nchi za Afrika Magharibi na
Afrika ya Kati zinaamini wanawake
katika soka ni nuksi na wanahusishwa na ushirikina,”alisema mlinzi mmoja wa uwanja huo.
katika soka ni nuksi na wanahusishwa na ushirikina,”alisema mlinzi mmoja wa uwanja huo.
Hata hivyo kamishna anayehusika na usawa wa jinsia
katika Kamati inayoshughulikia kuandaa fainali hizo, Javu Baloyo
alisema imani hizo za kishirikina hazina nafasi na wanawake wasizuiwe.
“Wanawake wanaenda katika mechi za soka kwa ajili
ya kushangilia timu zao na siyo kuwasumbua wachezaji, kushinda au
kupoteza mechi hakutakiwi kuhusisha wanawake,”alisema Baloyo.
Shabiki mmoja wa kike wa soka wa Afrika Kusini
alisema,”kitendo kilichofanywa cha kutuzuia kuwa huru uwanjani siyo
sahihi, pia wanawake tumeshushwa hadhi zetu, tumetukanwa na tunaona
tumerudishwa katika enzi zile za ubaguzi wa rangi.”
Naye ‘Sangoma’ mganga mmoja wa kienyeji nchini
Afrika Kusini anayeitwa, Bhayilatsholoza Mngambe alisema,”wanawake
wanatakiwa kuzuiwa kabisa kuingia viwanjani, kwa mujibu wa tamaduni za
kiafrika, wanawake hawatakiwi kuwa karibu na wanajeshi wakati wa vita,
Fainali za Afrika ni sawa na vita.”
- Kenya yahoji kauli ya Obama
- Waliotaka kuiba kwa Makamba watiwa mbaroni
- CCM Arusha yachachamaa uchaguzi Nec Longido
- John Mnyika: Sheria mpya zinawalinda mafisadi
- Koplo adaiwa kutapeli Sh45 milioni
- Waziri mkuu ataka wananchi washirikishwe
- Rushwa yagubika ugawaji mahindi ya chakula
- Wanaouza dawa za Serikali kukiona
- Rais Kikwete kutaja wajumbe Kamati Kuu
- RIPOTI MAALUMU: Utalii wa ngono waingia nchini
- Kamati ya Zitto yafutwa
- Bunge laibua ufisadi wa kutisha serikalini
- Mtwara wamkana Pinda
- Chadema kuwashtaki Makinda, Ndugai
- Chanjo ya Ukimwi yagunduliwa nchini
- RIPOTI MAALUMU: Utalii wa ngono waingia nchini
- Waganga feki wanavyochota mamilioni
- Luninga hupoteza nguvu za kiume
- Njaa yapeleka wananchi Zambia kufuata unga
- Yanga SC yaamriwa kulipa 106 mil