Saturday, April 27

Arsenal yasaka nafasi ya klabu bingwa ulaya dhidi ya Man U inayotaka kuweka recodi mpya.

United iliivua ubingwa City, na mchezo na Arsenal hawana cha kupoteza zaidi ya kulinda heshima.
London, England. KochaArsene Wenger amesema haoni shida kuwaambia wachezaji wake kujipanga na kuwapongeza wenzao wa Manchester United kwa kutwaa taji la Ligi Kuu England, lakini amepania kuhakikisha mabingwa hao wapya wanaondoka Uwanja wa Emirates wakiinamisha vichwa chini.
United inakwenda kwenye dimba la Emirates leo katika mchezo wa Ligi Kuu, huku mshambuliaji Robin Van Persie akirejea kwenye uwanja wake wa zamani alikokuwa nahodha kabla ya kujiunga na United.
United inataka kutumia mechi hiyo kama sehemu ya
kunogesha sherehe ya kutwaa taji la 20 England, lakini hilo likiwezekana kwa kuifunga Arsenal iliyojizatiti kuitubulia United.
Ingawa macho yatakuwa zaidi kwa Robin, sehemu nyingine ya mchezo huo inatarajiwa kujaza ushindani mkubwa.
United iliivua ubingwa Manchester City, na kwenye mchezo wao dhidi ya Arsenal hawana cha kupoteza zaidi ya kulinda heshima na kutaka kuweka rekodi.
Tofauti kwa Arsenal, ushindi kwao ni lazima ili kujiweka kwenye nafasi nzuri ya kuwania nafasi nne za juu kwenye msimamo.
City imejiimarisha vizuri kwenye nafasi ya pili na kazi kubwa iko kwa Arsenal inayowania kumaliza katika nafasi ya tatu, sambamba na Chelsea watakaocheza na Swansea kwenye uwanja wao wa nyumbani leo na Tottenham wanaoshika nafasi ya tatu, ambao jana walikuwa dimbani kucheza na Wigan.
Arsenal wako pointi moja mbele ya Chelsea na mbili mbele ya Tottenham na wanatarajia kujiimarisha zaidi kwa kuifunga United.
Baadhi ya mashabiki wa Arsenal wamechukizwa na uamuzi wa Wenger kuwaruhusu wachezaji wake kuwapa heshima United kwa kutwaa taji kabla ya mchezo wa leo, ikiwa ni marejeo kama hayo yaliyofanywa na wachezaji wa kikosi cha Alex Ferguson kilichowapa heshima Gunners walipotwaa ubingwa mwaka 1991.
Mashabiki hao wa Arsenal walisema kama uamuzi wa kocha Wenger utabaki kama ulivyo, basi watageuza migongo yao uwanjani wakati wachezaji wa United watakapopewa heshima.